Helping Hands International -Tanzania

Friday, November 18, 2016

HELPING HANDS INTERNATIONAL NI NINI?






Helping Hands International kwa kifupi ni (H2i) ni asasi isiyo ya kiserikali (NGO) ya kimataifa inayojihusisha na kusaidia kundi  la watu wenye mahitaji maalum (kama yatima,wajane, walemavu, waishio katika mazingira magumu)

Mbeba maono wa H2i ni Mama Luzviminda  Mac Elvis, kutoka nchini ya  Ufilipino ambaye   baada ya kupitia maisha magumu sana mwanzoni kutokana na kuzaliwa katika familia duni sana kiasi cha kujikuta anasomeshwa na mtu kutoka Marekani  ambaye  hata hakumfahamu kabisa,jambo lililomfanya aamini  kuwa licha ya matatizo anayoweza kukutana nayo binadamu yeyote akipata  mkono wa msaada anaweza  kutimiza ndoto zake.
Imani hii ilimfanya atafakari sana juu ya watu wenye matatizo kama aliyoyapitia yeye  na ikampelekea  kuanzisha mpango wa kuwasaidia, baada ya yeye  kuwa amefanikiwa kutokana na kusaidiwa, akiwa amehitimu masomo yake na  kuajiriwa kwa miaka mingi  Marekani alikeleketwa na maono yake ya muda mrefu aliamua kurejea kwao  Ufilipino na kuasisi asasi aliyoiita HELPING HANDS.
Asasi hii ilijihusisha na kuwasaidia watoto wa mitaani kurejea shule,kusomesha watoto yatima, wajane na wanaoishi katika mazingira magumu kuwasaidia kuanzisha miradi itakayowafanya wajitegemee na kuishi maisha mazuri
Akiwa anaendelea na kazi zake alikutana na Daktari Ramiel  Policarpio,ambaye  alikuwa ni daktari bingwa wa meno huko nchini Ufilipino. Naye alikuwa na maono yanayokaribiana sana na ya mama Luzviminda. Dr Ramiel  alikuwa inajihusisha na kusaidia ,wazee na wasiojiweza  katika nchi hiyo. Walipokutana wakabaini kuwa maono yao yanafanana na kwamba kwa pamoja wanaguswa na makundi yenye mahitaji maalumu hivyo waliamua kuunganisha nguvu na kuamua  kueneza huduma zao nje ya Ufilipino,yaani asasi ikawa ya kimataifa, na hapa ndipo jina  la asasi hii likabadilika na kuwa Helping Hands International  badala ya *Helping Hands* kama ilivyokuwa awali. Wakaanza kuenea barani Asia kwa kasi sana kutokana na mguso wa huduma zao kwa jamii. Jambo hili liliwafanya wakabiliwe na changamoto za kifedha ili kuwasaidia watu wengi waliojitokeza kutokana na udhamini wa awali kuzidiwa kabisa. Katika kutafuta suluhu kwa changamoto hii  waliamua kubuni  na kutafuta vyanzo vya mapato ili kuinua na kuendeleza  huduma hizi.

Kwa kawaida,Asasi nyingi zisizo za kiserikali (NGO) za kimataifa ama za kitaifa huendesha shughuli zake za kila siku kwa ufadhili wa makundi mbalimbali kama vile Serikali , makampuni ya kibiashara ya kimataifa, wafanyabiashara wakubwa ambao wanatoa misaada kwa jamii ( philanthropists), hivyo basi  H2i  yenyewe iliamua kutafuta makampuni makubwa ya kibiashara, ambayo  imefanya nayo makubaliano (partnership agreement) nayo ni  kampuni ya magari ya Hyundai-Korea Kusini, kampuni za computer za HP na Apple za Marekani, na kwa Nigeria ambako H2i ndio imeanzia kufungua ofisi  katika  bara la Africa huko kuna kampuni kama  Diamond Bank,GAC Motors, Glo nk

Pia ,waliamua kubuni chanzo kingine cha mapato ambacho kinatokana na michango  ya wanachama ( Help Partners) ambao wanajiunga  kwa hiari yao  baada ya kuguswa  na matatizo ya watu waliolengwa na asasi hii na kuamua kuwa sehemu ya utekelezaji wa maono. Hivyo ikapangwa kuwa mtu yeyote anayetaka kuwa Help partner katika nchi yeyote  duniani basi sharti atoe kiingilio cha (dollar) $40 ( kwa wakati huu ni sawa  na sh 90,000/=) Fedha hii ikitolewa hairudishwi (non refundable). Mchango huu unatolewa mara moja tu na Help partner na uanachama ni wa kudumu.  Pamoja na kuwa kiingilio kinaonekana kidogo lakini kwa sababu ya uwingi wa Help partners waliopo katika nchi mbalimbali,  kiwango hicho  kinakuwa kikubwa na hivyo kuweka kufadhili shughuli za asasi

Ili kuwafikia walengwa {yatima na wajane} popote duniani  asasi inawatumia Help partners. Help partner ni mtu ambaye ameyaelewa maono ya asasi na ameaumua kwa hiari yake mwenyewe kuwa sehemu ya kutekeleza maono  hayo yaani kuwafikia na kuyasaidia hayo makundi husika na ametoa kiingilio na amejiunga kwa kutoa sh 90,000 ( sawa na $ 40)

JE HELP PARTNER ANAFAIDIKAJE?
1) Asasi inawatumia Help partners wake kuwafikia walengwa {makundi ya yatima,wajane }
2)Mpango wa uwezeshwaji wa H2i. Asasi hii kwa makusudi na kimkakati  kabisa imeamua kuwawezesha Help partners wote kiuchumi   

HUDUMA TANO ZINAZOTOLEWA NA H2i KWA WANACHAMA WAKE [HELP PARTNER]
[Kitendo cha wewe kuamua kuwa  Help partner basi  moja kwa moja unanufaika na huduma 5 zifuatazo]
1. HUDUMA YA MISAADA YA KIBINADAMU { HUMANITARIAN SERVICES }
Kuwasaidia  yatima,wajane nk- Help partner ndiye  anayependekeza yatima, au wajane/kituo cha yatima, wazee wasiojiweza nk  yaani makundi  ambayo yatasaidiwa na  H2i (Msaada utatolewa kwa niaba yake  
2.HUDUMA YA UWEZESHWAJI WA KIUCHUMI {FINANCIAL EMPOWERMENT SERVICES}
Mtu yeyote anapoamua kujiunga na kupata usajili wa kuwa Help partner, anaingizwa moja kwa moja  kwenye mfumo wa kupata fedha kama bonus mbalimbali  kwa kadiri unavyopanda vyeo katika Asasi hii.[Kuna cheo cha 1 mpaka 6 ]  Pia unapata zawadi za vitu vya thamani kama Laptop, ipad, magari, mkopo wa nyumba, mkopo wa biashara .
Kigezo cha Help partner kuanza kufaidi huduma hii ni lazima uwashirikishe watu wengine fursa hii,unatakiwa uwashawishi watu wasiopungua wawili kujiunga na Asasi hii
3. HUDUMA YA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI {TRADE & SKILL ACQUISITION SERVICES}
Asasi hii inatambua umuhimu wa kumwendeleza Help partner, kwa hiyo utapata fursa ya kujifunza  ujasiliamali na biashara. Utafundishwa  ujasiriamali wa kutengeneza vitu mbalimbali kama rangi za nyumba, sabuni nk, pia kujifunza kutunza kumbukumbu za kifedha
( Utapata huduma hii utakapokuwa kwenye cheo cha 3).
4. HUDUMA YA MALI NA RASILIMALI  {ASSETS & PROPERTY ACQUISITION SERVICES}
Help partner anaruhusiwa kukopa au kununua nyumba  au kitendea kazi chochote ( Masharti yote ya ukopaji yatazingatiwa) mkopo hauna riba na unarudishwa ndani ya mwaka mmoja ( Hii inatolewa kwa wale waliofika cheo cha 4 na 5)
5: HUDUMA YA UFADHILI WA MASOMO KWA WATOTO WAKO ( SCHOLARSHIP AWARD SERVICES)
Kila Help partner atakeyeingia kwenye cheo cha 5 kwenye Asasi  hii atapewa ada ya watoto wake  2, bila kujali kwamba ana watoto au watoto wake ni wakubwa wanajitegemea  au la


H2i INATUMIA MFUMO WA  BIASHARA YA MTANDAO {NETWORK MARKETING}
Ili kuhakikisha kwamba taasisi inasambaa  katika nchi mbalimbali  duniani yaani wanapata Help partners wengi kwa kadiri inavyowezekana  na hivyo  kuwafikia walengwa wengi zaidi (yaani wajane,yatima, walio katika mazingira magumu) na kuhakikisha kwamba fedha ya kuwafadhili walengwa inayotolewa kama kiingilio inaongezeka na hakuna ukwasi basi  H2i ilibuni na kuamua kutumia  mfumo wa biashara ya mtandao ( Referal Marketing /Network marketing).
ü  Biashara ya mtandao ni ya kupashana habari kati ya  mtu na mtu, yaani  unawashikisha  fursa rafiki zako, jirani zako, waumini wenzio nk. Hivyo basi baada ya wewe kujiunga utatakiwa kuwashirika watu wasiopungua wawili  wengine ambao nao pia watatakiwa watawatafute watu wawili na kuendelea. Huzuiwi kuingiza idadi yoyote ya watu uliyonayo hata kama ni watu 100! japo kiwango cha chini sana ni watu wawili.
(maelezo ya kina ya  namna unavyoweza kupanda cheo toka cha 1hadi cha 6 itafuata)

Huu ni mfumo huu wa biashara ulionekana ni bora sana na rahisi kufanya. Asasi hii ilianza kuenea na kupanuka na ikatoka  nje na Asia na mnamo mwaka  Desemba 2013 H2i ilipoingia Afrika kituo kikawa Lagos, Nigeria,
African Region Corporate Office
Jonathan Goodluck Estate
Cluster 26B, Flat 2
Isheri Olofin Alimosho LGA
Egbeda, Lagos, Nigeria
Kwa sasa Helping Hands International inaenea kwa kasi katika nchi za Africa, tayari ipo  Benin,Ethiopia, Uganda,Kenya,Afrika Kusini,Ghana,Zambia,Msumbiji,Zimbabwe na hatimaye Tanzania. Hapa kwetu Tanzania uzinduzi kitaifa umefanyika mwezi wa saba Mwaka huu japo watu walianza kufanya kazi kabla ya uzinduzi.

Kwa ufafanuzi zaidi  kuhusu Asasi hii / Kujiunga
Tembelea  tovuti:  www.helpinghandsinternational.biz
                         www.facebook.com/HelpinghandsInternationalTanzania
                         www.helpinghandsinternationaltanzania.blogspot.com

  Call +255 622 673 000    Whatsapp +255 712 673 000   Email: help2i.Tanzania@gmail.com

Image result for whatsapp symbols

No comments:

Post a Comment